
Leo naleta hoja nzito kidogo. Najua baadhi ya akina dada watakwazika. Kwa hiyo, naomba mnisamehe.
Siku hizi limezuka wimbi la akina dada na hata akina mama kujilemba kwa
namna mbalimbali kuanzia rangi ya mwili, nywele, kucha, midomo na
wengine wamefikia hatua ya kunywa au kupaka dawa za kichina za kuongeza
makalio na maziwa. Wengine wanasuka nywele ndefu na wanaongea kwa
mbwembwe huku wanatikisa vichwa vyao na kushikashika nywele kama
wafanyavyo wanawake wa kizungu. Wengine wamefikia hatua ya kubadili hata
sauti na namna ya kuongea!!
Najua dada zetu wanafanya hivyo kwa lengo la kupendeza na wengine lengo
lao ni kuwavutia wanaume. Lakini mimi binafsi sijui ni nini kimenitokea!
Inawezekana ndiyo abnomality hiyo. Kadri mwanamke anavyojilemba zaidi
ndivyo hamu ya kufanya nae mapenzi inavyopungua.
Ukweli ni kwamba nikilala na mwanamke ambaye ni natural yaani mwenye
nywele za kawaida anayesuka mtindo wa 'twende kilioni' au amezibana tu,
wowowo, chuchu na sauti natural huwa napata nguvu nyingi za kupanda
mlima ikilinganishwa na ninapolala na mwanamke mwenye kucha za bandia,
nywele za bandia, na midomo iliyopakwa rangi nyingi.
Sijui ni ugonjwa au ni jambo ambalo hata wanaume wenzangu huwa linawakumba?