Taarifa zinadai kuwa wanandoa hao wapya walipanga kufunga ndoa hiyo huko Chateau de Versailles lakini sheria za Ufaransa hazikuwaruhusu kufanya hivyo kutokana na hata mmoja wao kutokuwa na uraia wa nchi hiyo.
Cha kushangaza ni kwamba si Jay Z wala Mke wake Beyonce aliyehudhuria katika harusi hiyo na kuishia kutuma salamu za pongezi licha ya kuwepo kwa uvumi kuwa Jay Z atakuwa msimamizi wake kutokana na ukaribu na urafiki mkubwa waliokuwa nao.
Tukio hilo kubwa limehudhuriwa na wageni mbalimbali na watu mashuhuri akiwemo mwanamuziki John Legend na mkewe Chrissy Teigen na muongozaji wa filamu ya 12 Years a Slave Steve McQueen.
Story nyingine kubwa ni kwamba mabosi wa kampuni ya Adidas pia walichagua siku hiyo ya harusi kuzindua tangazo lao la kombe la dunia kwa mwaka 2014 linalomhusisha rapa Kanye West pamoja na mastaa wakubwa wa soka duniani Lionel Messi na Dani Alves.