Saturday, June 7, 2014

Hii ni Collabo Nyingine ya Kimataifa Atakayofanya Diamond

0

Nafasi moja huanzisha nyingine. Diamond hakwepeki kwenye vichwa vya habari hivi sasa kwa kuwa mengi mazuri yanaendelea juu yake.Ikiwa leo usiku tutashuhudia utoaji wa tuzo za MTV hapa jijini Durban (ambapo Sammisago.com ipo), jana wasanii wanaoshiriki katika tuzo hizo akiwemo Diamond walifanya Press Comference iliyoandaliwa na MTV na kuzungumzia mengi.
Lakini kikwetukwetu, Diamond ametajwa na kundi la Mafikizolo la Afrika Kusini kuwa ni msanii ambaye wanazungumza nae kwa ajili ya kufanya wimbo wa pamoja.
Kwa hiyo kuna mlolongo wa nyimbo za collabo za kimataida zitakuja kutoka kwa Diamond. Hivi karibuni alikuwa Nigeria na alimshirikisha Iyanya na Tiwa Savage, na inawezekana kukawa na surprise ya collabo na msanii mkubwa wa Marekani.
Author Image

About tzfleva
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design

No comments:

Post a Comment