P Diddy anaweza kuwa msanii wa kwanza wa Hiphop kuwa billionea kwenye miaka michache ijayo kutokana na kasi yake ya kuingiza pesa nyingi na uwekezaji wenye faida kubwa nje ya muziki.
Namba moja kwenye hii listi imekamatwa na P.Diddy ambaye kutokana na mkataba wake mpya na kampuni ya Diageo ambapo bado anahusika na usimamizi wa brand ya Ciroc lakini pia DeLeon Tequila imeongezeka na kuongeza mapato kwake.
Revolt TV anayomiliki P Diddy ambayo imeanza kwa kasi kubwa ndiyo biashara inayosemekana kuwa inaweza kumfanya Diddy kubwa bilionea wa kwanza kwenye HipHop.
Mwaka jana alikuwa na utajari wa dola millioni 580 lakini ndani ya mwaka mmoja ameingiza dola millioni 120 na kufanya utajiri wake kuwa na jumla ya dola za kimarekani millioni 700.