Sunday, July 6, 2014

Linex Kuhusu Wimbo Aliomshirikisha Diamond

0
Msanii wa bongo fleva kutoka Kigoma Linex Aka Leka Meka amesema kazi aliyofanya na Diamond ‘Salima’ itatoka baada ya kuachia wimbo wake alioupa jina ‘Wema Kwa Ubaya’.
Linex kwenye Interview na sammisago.com anasema wimbo wake wa Wema Kwa Ubaya video imeshalipiwa na Mhe Zitto Kabwe kwa Adam Juma na kwamba muda wowote itatoka.
Kuhusu kazi aliyofanya na Diamond, Linex ameweka wazi kuwa ni kazi itakayolenga level za kimataifa zaidi.
“Ni muda wa kufanya mambo makubwa zaidi kwenye muziki na imani yangu ni kuwa kazi hii niliyofanya na Diamond ‘Salima’ itafanya vizuri kama itakuwa na video bora na usimamizi mzuri nje na ndani ya Bongo”
Linex ni miongoni mwa wasanii wanaojituma sana Tanzania na utakumbuka kuwa aliwahi kumlipa zaidi ya Milioni moja Video Queen Jackie Cliff ilikuigiza kwenye video yake ya Kimugina.
Author Image

About tzfleva
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design

No comments:

Post a Comment