Mpaka timu zinaenda mapumziko Tanzania ilikuwa mbele kwa goli 4-0,goli pekee la Marekani katika mchezo huo ambayo hadi nusu fainali ilikuwa haijafungwa lilifungwa dakika za mwisho za mchezo huo.
Kwa matokeo haya Tanzania inacheza nusu fainali na Burundi,Mechi hiyo inachezwa leo (Aprili 6 mwaka huu) ambapo Burundi imetinga hatua hiyo baada ya kuifunga Pakistan goli 4-3 katika nusu fainali ya pili.
Mchezo huo wa fainali unachezwa uwanja mkongwe na maarufu wa klabu ya Fluminense katikati ya Jiji la Rio de Janeiro huku mgeni rasmi akiwa Waziri wa Fedha wa Uingereza George Osborne.
Katika mechi ya kwanza katika kundi B la michuano hiyo,Tanzania ilicheza na Burundi na kutoka sare ya mabao 2-2.